Pamoja na kupambana na maambukizi ya virusi vya Korona Marjaa Dini mkuu amesisitiza kua: Kuwatibu wagonjwa na kuwahudumia ni wajibu kifaya, atakaejitolea uhai wake atapata thawabu za shahidi.

Maoni katika picha
Marjaa Dini mkuu amesisitiza kua kuwatibu wagonjwa na kuwahudumia ni wajibu kifaya kwa kila mwenye uwezo wa kufanya hivyo ambao ni madaktari, wauguzi na wengineo, serikali inatakiwa iwape vifaa vyote vinavyo hitajika kwa ajili ya kuwalinda na maambukizi, wala haitakiwi kutoa udhuru katika hilo, atakaejitolea maisha yake kwa ajili ya kumhudumia mgonjwa ataandikiwa thawabu za shahidi.

Hayo yapo kwenye jibu la Mheshimiwa Marjaa Dini mkuu Ayatullah Sayyid Hussein Sistani la swali lililotumwa kwenye ofisi yake.

Tazama pisha iliyo ambatana na habari hii kuona jibu kamili.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: