Kwa mara ya pili ndani ya wiki moja: Katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya tukufu ameutembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha kuhudumia watu walio ambukizwa virusi vya Korona katika hospitali ya Hindiyya

Maoni katika picha
Katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya tukufu Mhandisi Muhammad Ashiqar asubuhi ya leo suku ya Jumapili mwezi (18 Shabani 1441h) sawa na tarehe (12 Aprili 2020m), ametembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha watu walio ambukizwa virusi vya Korona, kinacho jengwa na mafundi wa kitengo cha usimamizi wa kihandisi katika Atabatu Abbasiyya tukufu kwenye eneo la hospitali ya Hindiyya, wamejitolea kujenga kituo hicho kama sehemu ya kupambana na ugonjwa wa Korona.

Katibu mkuu huyo amefuatana na jopo la wajumbe wa kamati kuu ya uongozi, wameangalia maendeleo ya kazi na kusikiliza maelezo kutoka kwa watendaji pamoja na changamoto zao.

Katibu mkuu ameshukuru kazi nzuri inayo fanywa na mafundi hao kwaniaba ya Kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya pamoja na watumishi wa Ataba, akasema kua: “Atabatu Abbasiyya inajenga kituo hiki kutokana na maelekezo ya Marjaa Dini mkuu, aliyehimiza kusaidia sekta ya afya pamoja na watu wanaosimama imara kuhudumia wagonjwa wa Korona, kila tatizo linalo tokea katika taifa letu Ataba tukufu husaidia kupambana nalo, ikiwa ni pamoja na tatizo hili la kiafya, haijajifunga kwenye kuhudumia mazuwaru peke yake bali inahudumia jamii yote, kituo hiki tunacho jenga katika mji wa Towareji kwenye hospitali kuu ya Hindiyya ni moja ya mchango wentu katika kuhudumia jamii, tunamshukuru Mwenyezi Mungu mtukufu kwa maendeleo makubwa tunayo shuhudia, mafundi wa kitengo cha usimamizi wa kihandisi wamepiga hatua kubwa katika ujenzi wa kituo hiki”.

Kumbuka kua mafundi wa kitengo cha usimamizi wa kihandisi katika Atabatu Abbasiyya tukufu walianza ujenzi wa kituo hiki siku ya mwezi (6 Shabani 1441h) sawa na tarehe (31 Machi 2020m), kama sehemu ya mchango wao katika kupambana na virusi vya Korona, kituo kinajengwa kwenye kiwanja chenye ukubwa wa (2m1500) kitakua na vyumba vya wagonjwa 35 pamoja na chumba cha kutunzia vifaa vya usafi na chumba cha dawa.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: