Kwa mara ya pili: Chuo kikuu cha Al-Ameed kimepunguza ada za masomo

Maoni katika picha
Chuo kikuu cha Al-Ameed ambacho kipo chini ya kamati ya malezi na elimu ya juu katika Atabatu Abbasiyya tukufu, kimepunguza ada za masomo kwa asilimia (%10) katika michepuo na hatua zote za masomo ya mwaka (2019/2020m) ikiwa ni mara ya pili ndani ya mwaka mmoja.

Punguzo hilo ni sehemu ya kuonyesha mshikamano na wanafunzi wake kutokana na mazingira magumu ambao wananchi wanapitia kwa sasa, punguzo lipo kama ifuatavyo:

  • 1- Ada ya masomo katika ngazi zote imepunguzwa mara ya pili kwa asilimia kumi (%10), katika mwaka wa masomo (2019/2020m).
  • 2- Hivyo jumla ya punguzo katika mwaka wa masomo (2019/2020m) linakuwa asilimia ishirini (%20).
  • 3- Mwanafunzi atanufaika na punguzo hilo (lililo tajwa kwenye namba moja) kwa kulipa ada kamili ya masomo kuanzia tarehe (29/04/2020m) hadi mwisho wa mda rasmi wa kazi katika siku ya Jumatano ya tarehe (20/05/2020m).
  • 4- Punguzo la pili (lililo tajwa kwenye namba mbili) halihusishi wanafunzi waliopewa punguzo hapo awali kwa sababu maamum.
  • 5- Wanafunzi watakao chelewa kulipa ada zao baada ya tarehe (20/05/2020m) hawatapewa punguzo lililotajwa kwenye namba moja.
  • 6- Mwanafunzi aliyelipa pesa kamili katika muhula wa kwanza wa mwaka wa masomo ambao punguzo lake ni asilimia tano (%5) pesa hiyo itaongezwa kwenye muhula wa kwanza wa mwaka ujao wa masomo.

Kumbuka kuwa wizara ya elimu ya juu na utafiti wa kielimu imekipongeza chuo kikuu cha Al-Ameed kwa kupunguza ada za masomo kwenye michepuo yake, kwani kufanya hivyo ni kuwasaidia wazazi wa wanafunzi, hayo yamo katika barua ya kukipongeza chuo hicho kutoka wizarani.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: