Kusambazwa kikosi cha Skaut (Aljawaalah) kwa ajili ya kupuliza dawa na kuongoza mawakibu za waombolezaji

Maoni katika picha
Kikosi cha mafunzo na uokozi Alkafeel kimesambaza Skaut (Aljawaalah) ndani na nje ya haram tukufu ya Abulfadhil Abbasi (a.s), kwa ajili ya kuwapuliza dawa watu wanaoshiriki kwenye mawakibu za waombolezaji, pamoja na kutoa maelekezo na kugawa vipeperushi vinavyo eleza hatari ya janga la Korona na namna ya kujikinga nalo.

Sayyid Murtadhwa Ghalibi amesema kuwa: “Kikosi chetu kimezowea katika kila msimu wa ziara zinazo hudhuriwa na mamilioni ya watu, husambazwa Skaut wa kitengo cha Aljawaalah kwa ajili ya kufanya shughuli za uokozi wa mazuwaru na kutoa msaada wa haraka utakao hitajika na zaairu, lakini mwaka huu kutokana na kuwepo janga la Korona kazi yake imetofautiana na miaka mingine, mwaka huu tunafanya mambo yafuatayo:

  • - Kushindikiza mawakibu za waombolezaji zinazo ingia katika malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s), na kupulizia dawa vikundi vya watu wanaoshiriki kwenye maukibu hizo, kwa kutumia dawa zilizo pasishwa na idara ya madaktari wa Ataba tukufu, kazi hiyo inaanzia wakati maukibu zinapo karibia kuingia ndani ya haram na inaendelea hadi zitakapo toka na kushindikizwa hadi kwenye uwanja wa katikati ya haram mbili takatifu.
  • - Kuna kikosi cha wanaskaut wa kitengo cha Aljawaalah waliopewa jukumu la kutoa elimu na kugawa vipeperushi vinavyo eleza hatari ya maambukizi ya virusi vya Korona na namna ya kujikinga navyo”.

Kumbuka kuwa kikosi cha mafunzo na uokozi kimesha okoa maisha ya mamia ya mazuwaru kwenye ziara zilizo pita na kuhakikisha usalama wao pamoja na kuweka mazingira rafiki, sambamba na kuzuwia misongamano ya mazuwaru, na kupeleka watu wenye matatizo ya afya kwenye hospitali za karibu kwa kutumia magari maalum ya wagonjwa.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: