Mambo yaliyo elekezwa ni:
- Lazima kuvaa soksi za mikononi wakati wa kufanya kazi kwenye maukibu na wakati wa kwenda kwenye majlisi za kuomboleza.
- Lazima kuvaa barakoa na kutumia vitakasa mikono muda wote pamoja na kupuliza dawa kwenye eneo la maukibu na husseiniyya.
- Kuheshimu umbali kati ya mtu na mtu wakati wa matembezi ya maukibu za waombolezaji na kwenye majlisi kama ilivyo elekezwa na idara ya afya.
- Upikaji wa chakula ufanywe ndani ya husseiniyya katika sehemu zilizo tengwa kwa ajili ya upishi ambazo zimekamilisha masharti ya afya.
- Ugawaji wa chakula na vinywaji kwa mazuwaru ufanywe kwa kutumia vifungashio (tak away) na vyombo vyenye mifuniko.
- Maukibu zitembee katika njia zilizo pangiwa.
- Kuandaa sehemu ya dharura ya kutolea huduma ya afya katika kila maukibu au kikundi, na kila maukibu iwe na watu (2-3) wenye jukumu la kuhimiza kuvaa barakoa na kutumia vitakasa mikono pamoja na kupuliza dawa na kutekeleza masharti yote ya idara ya afya.
- Inapasa kumzuwia mtu yeyote kushiriki kwenye maombolezo au majlisi ya Husseiniyya kama hajavaa soksi za mikononi na barakoa.