Kitengo cha habari katika Atabatu Abbasiyya tukufu kimetoa maelekezo kwa vyombo vya habari vitakavyo rusha matukio ya ziara ya Arubaini

Maoni katika picha
Kitengo cha habari katika Atabatu Abbasiyya tukufu, kimetoa maelekezo kwa vyombo vya habari vitakavyo rusha matukio ya ziara ya Arubaini mwaka huu, kimehimiza umuhimu wa kuheshimu maelekezo hayo kwa faida ya wote, na kuhakikisha tunatoa picha halisi ya ziara hii takatifu.

Makamo rais wa kitengo hicho Ustadh Muhammad Asadi amesema kuwa, maelekezo hayo ni:

  • - Kuzingatia sehemu na muda uliopangwa kupiga picha.
  • - Kutoa ushirikiano na idara za Ataba mbili tukufu Husseiniyya na Abbasiyya kwa ajili ya kulinda utukufu wa ziara.
  • - Atakae poteza kitambulisho au akachelewa kukabidhi atalipa faini ya dinari (250,000).
  • - Idara za Ataba mbili tukufu zinahaki ya kukagua kamera kabla na baada ya kupiga picha na zinahaki ya kufuta chochote zitakacho ona kinafaa kufutwa.
  • - Hairuhusiwi kufanya mahojiano ya mubashara au yasiyokua mubashara bila kujua idara za Ataba mbili tukufu.
  • - Hairuhusiwi kutoa kitambulisho nje ya eneo la uwanja wa katikati ya haram mbili tukufu, lazima urudishe kitambulisho baada ya kumaliza kupiga picha.
  • - Muandishi wa habari anatakiwa akabidhi kitambulisho chake cha uraia na cha chombo cha habari anacho fanyia kazi.
  • - Hairuhusiwi kupiga picha binafsi ndani ya maeneo tuliyo taja.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: