Makumbusho ya Alkafeel ya vifaa na nakala-kale imefungua milango ya kupokea watu wanaokuja kuitembelea kwa kufuata kanuni na maelekezo ya idara ya afya

Maoni katika picha
Makumbusho ya Alkafeel katika Atabatu Abbasiyya tukufu imetangaza kufungua milango kwa mazuwaru wake chini ya kanuni na maelekezo ya idara ya afya, kwa ajili ya kulinda usalama wa wageni na watumishi wake, baada ya kufungwa kwa zaidi ya miezi kumi kwa sababu ya janga la virusi vya Korona, na kutekeleza maagizo ya mamlaka za afya sambamba na kuheshimu umbali unaotakiwa kati ya mtu na mtu.

Haya yamethibitishwa kwenye mtandao wa Alkafeel na rais wa kitengo cha makumbusho Ustadh Swadiq Laazim, amesema: “Kutokana na maelekezo ya uongozi mkuu wa Atabatu Abbasiyya tukufu ya kufungua makumbusho ya Alkafeel baada ya kufungwa kwa muda mrefu kwa sababu ya janga la maambukizi ya virusi vya Korona, tumechukua hatua za kujilinda na maambukizi kwa ajili ya kulinda usalama wa mazuwaru na watumishi wa makumbusho, tunafuata maelekezo yote yaliyotolewa na idara ya afya”.

Miongoni mwa mambo yatakayo zingatiwa ni:

  • - Watu wataingia kwa utaratibu maalum wakiwa wamesimama umbali unaotakiwa kati ya mtu na mtu na kuhakikisha hakutokea msongamano.
  • - Dawa itapulizwa wakati wote katika sehemu zote za makumbusho.
  • - Kutakuwa na sehemu maalum za kupulizwa dawa mazuwaru ndani ya makumbusho.
  • - Watawekwa watumishi watakao ongoza utembeaji wa mazuwaru ndani ya makumbusho, ili kuhakikisha misafara ya mazuwaru haisimami sana na kusababisha msongamano.

Kumbuka kuwa baada ya kutokea janga la maambukizi ya virusi vya Korona, makumbusho ilifungwa chini ya maelekezo ya idara ya afya, na sasa hivi baada ya kurudi harakati za mazuwaru chini ya kanuni na maelekezo ya idara ya afya, makumbusho nayo imefunguliwa, kwani huzingatiwa moja ya vituo muhimu vya mazuwaru baada ya kumaliza ibada ya ziara.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: