Idara ya Quráni inafanya shindano la (Jua nyuma ya mawingu) kwa wanawake

Maoni katika picha
Idara ya Quráni chini ya ofisi ya maelekezo ya Dini kwa wanawake, inayo fungamana na ofisi ya katibu mkuu wa Atabatu Abbasiyya tukufu inafanya shindano liitwalo (Jua nyuma ya mawingu) kwa wanawake tu.

Shindano hili linafanywa sambamba na kuadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa Imamu wa zama (a.f) likiwa na maswali ishirini kuhusu uhai wake.

Sharti la kushiriki kwenye shindano hili, mshiriki hatakiwi kuwa na umri chini ya miaka (18), shindano litafanyika kwa muda wa siku mbili.

Ili kushiriki kwenye shindano ingia kupitia link ifuatayo: https://forms.gle/4qofUdPqH8NW4UuGA

Kumbuka kuwa lengo la shindano hili ni kuitambulisha historia ya Maimamu watakatifu (a.s) na kufanyia kazi maneno yao na vitendo vyao pamoja na kufuata mwenendo wao.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: