Picha za sasa hivi katika matembezi ya Towareji, yaliyo anza baada ya swala ya Adhuhuri ya leo siku ya Alkhamisi mwezi kumi Muharam (1443h) sawa na (19 Agosti 2021m).
Tambua kuwa matembezi ya Towareji ni utamaduni uliozoweleka wa kuomboleza siku ya Ashura, ulianzishwa na watu wa Towareji (wilaya ya Hindiyya katika mkoa wa Karbala, kilometa 20 kutoka makao makuu ya mkoa), kama sehemu ya kuitikia wito wa Imamu Hussein (a.s) aliotoa siku ya mwezi kumi Muharam (Je kuna wakunusuru aninusuru?), ni miongoni mwa matembezi yanayo husisha watu wengi zaidi duniani, yalianza mwaka (1303h) sawa na mwaka (1885m).