Muhimu.. ofisi ya Sayyid Sistani imetangaza kuwa kesho siku ya Jumatano ni siku ya kwanza ya Idul-Fitri.

Ofisi ya Muheshimiwa Marjaa-Dini mkuu Ayatullah Sayyid Ali Husseini Sistani imetangaza kuwa kesho siku ya Jumatano ya tarehe 10 Aprili ni siku ya kwanza ya Idul-Fitri.

Ofisi ya Sayyid Sistani imesema “Imethibiti kuandama kwa mwezi kisheria hapa Iraq na maeneo yote ya miji hii, hivyo Jumatano ya kesho ni siku ya kwanza ya Idul-Fiti mwezi mosi Shawwal mwaka 1445h”.

Akaongeza kuwa “Tunamuomba Mwenyezi Mungu mtukufu awakubalie wote funga na swala zao na atupe amani furaha na baraka katika sikukuu hii tukufu”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: