Maukibu ya watu wa Karbala inaomboleza kifo cha Bibi Zaharaa (a.s) katika mji wa Najafu.

Maukibu ya watu wa Karbala imeomboleza kifo cha Bibi Fatuma Zaharaa (a.s) katika mji wa Najafu kwa mujibu wa riwaya ya tatu.

Makamo rais wa kitengo cha maadhimisho na mawakibu Husseiniyya Sayyid Ahmadi Shakiri amesema “Watu wa Karbala wamezowea kuomboleza kifo cha mbora wa wanawake duniani (a.s) katika mji wa Najafu, ili kumpa pole Imamu Ali (a.s)”.

Akaongeza kuwa “Maukibu ya kuomboleza hufanywa na watu wa Karbala kila mwaka kwa kushirikiana na Atabatu Abbasiyya tukufu”.

Watu wa Karbala hufanya mawakibu za kuomboleza pamoja na majaalisi za kuwataja Ahlulbait (a.s) na kuhuisha elimu na utukufu wao.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: