Sayyid Dhiyaau-Dini amepongeza kazi zinazofanywa na taasisi hiyo, ya kulea mayatima kutoka mikoa tofauti ya Iraq, akasisitiza kuendelea kwa ushirikiano baina ya Ataba na taasisi ya Ain kwa ajili ya malengo ya kibinaadamu yanayonufaisha jamii.
Kiongozi wa tawi la taasisi katika mkoa wa Karbala, Sayyid Hassan Alawi amesema “Ziara hii ni sehemu ya kutoa shukrani kwa Atabatu Abbasiyya tukufu kutokana na ushirikiano wake mkubwa katika kuhudumia jamii”.
Kikao kikahitimishwa kwa kumkabidhi ngao katibu mkuu, kama sehemu ya kupongeza mchango wa Ataba tukufu katika kuisaidia taasisi ya Ain misaada ya kibinaadamu na kijamii.



