Vitalu vya Alkafeel vimeadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa Imamu Hassan (a.s)

Vitalu vya Alkafeel chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu, vimeadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa Imamu Hassan Almujtaba (a.s) kwa kufanya hafla kubwa.

Kiongozi wa vitalu Sayyid Muhammad Harbi amesema “Atabatu Abbasiyya tukufu imeandaa hafla mbalimbali za kuadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa Imamu Hassan Almujtaba (a.s) kwenye maeneo tofauti, likiwemo eneo la vitalu vya Alkafeel”.

Akaongeza kuwa “Hafla imepambwa na usomaji wa tenzi, qaswida na mashairi kutoka kwa waimbaji mahiri mbele ya familia za watu wa Karbala sambamba na utoaji wa zawadi za maua kwa wahudhuriaji”.

Akasema kuwa “Atabatu Abbasiyya huadhimisha matukio yanayohusu Ahlulbait (a.s)”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: