Muheshimiwa Sayyid Swafi amempa zawadi mwanafunzi Zahara Haidari mwenye mahitaji maalum katika hafla ya wahitimu mabinti wa Alkafeel awamu ya tisa

Kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya Muheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi, amempa zawadi mwanafunzi mwenye mahitaji maalum Zahara Haidari, katika mahafali ya wahitimu wa vyuo vikuu vya Iraq na nchi za kiislamu (awamu ya tisa).

Mahafali imeandaliwa na idara ya shule za wasichana Alkafeel chini ya ofisi ya kiongozi mkuu wa kisheria katika Ataba takatifu, ikiwa na kauli mbiu isemayo (Kutokana na nuru ya Fatuma –a.s- tunaangaza ulimwengu), kwa ushiriki wa wanafunzi elfu 5 kutoka vyuo vikuu tofauti vya Iraq na baadhi ya nchi za kiarabu na kiislamu.

Utoaji wa zawadi hiyo ni sehemu ya kujenga hamasa kwa wahitimu, kwani ni ujumbe wa wazi kwa wote kuwa hakuna kisichowezekana, kila kikwazo kinaweza kuwa hatua ya kuelekea kwenye mafanikio.

Atabatu Abbasiyya tukufu hufanya mahafali ya wahitimu (mabinti wa Alkafeel), kwa lengo la kujenga hamasa kwa wahitimu wanaokamilisha safari ya masomo na kuanza maisha ya kufanya kazi wakiwa sehemu hii ya haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: