Majlisi imehudhuriwa na kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya Mheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi, katibu mkuu Sayyid Murtadha Aalu Dhiyaau-Dini na baadhi ya viongozi na watumishi wa Ataba, bila kusahau kundi kubwa la walimu wa hauza, wanafunzi, viongozi wa kidini, kijamii, waumini na waombolezaji.
Wahudhuriaji wametoa salam za rambirambi kwa ndugu na wapenzi wa marehemu, wamemuomba Mwenyezi Mungu amuweke mahala pema peponi marehemu na kuwatunuku subira na utulivu wafiwa.
Marjaa-Dini mkuu Ayatullah Sayyid Ali Husseini Sistani ametuma salam za rambirambi kutokana na kifo cha Ayatullah Shekhe Muhammad Is-haqa Alfayaadh (r.a), akapongeza kazi kubwa aliyofanya ya kutumikia hauza na kueneza elimu ya Ahlulbait (a.s).














