Kukabidhi bendera hiyo ni sehemu ya maandalizi ya kubadilisha bendera nyekundu na kuweka nyeusi jioni ya Jumanne kama ishara ya kuanza msimu wa huzuni na uombolezaji wa msiba wa Imamu Hussein na watu wa nyumbani kwake (a.s).
Ataba tukufu, jioni ya leo imeshuhudia ushiriki wa kundi kubwa la zuwaru kutoka ndani na nje ya Iraq, waliokuja katika shughuli ya kubadilisha bendera za malalo mbili takatifu ya Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s).
Ataba takatifu imefanya maandalizi makubwa, imepandisha bendera za uombolezaji kama ishara ya kupokea msimu wa huzuni mwezi wa Muharam na Safar.





