Kufunga semina ya saba ya kumtambua mwalimu mwenye mafanikio..

Maoni katika picha
Muendelezo wa semina zinazo endeshwa na idara ya mahusiano na vyuo vikuu katika Atabatu Abbasiyya tukufu, siku ya Juma Tano (30 Dhulqa’adah 1438h) sawa na (23 Agosti 2017m) katika ukumbi wa Imamu Mahdi (a.f) chini ya Atabatu Abbasiyya, ilifanyika hafla ya kufunga semina ya saba ya mwalimu mwenye mafanikio, iliyo kua na washiriki 36 kutoka katika vituo tofauti ndani ya mkoa wa Baabil kwa kushirikiana na mkuu wa kitengo cha malezi wa eneo hilo.

Semina hii ilikua ni sehemu ya kukamilisha semina zilizo pita, ilikua na maudhui nyindi zinazo muongezea mwalimu maarifa zaidi, na kumfanya kua na uweledi zaidi katika ufundishaji hasa unaoendana na maendeleo ya teknolojia za kisasa na kumfanya aeleweke kwa urahisi zaidi kwa wanafunzi pindi anapo fundisha, washiriki wamethibitisha kua semina hii inamatokeo chanya katika shuguli zao.

Miongoni mwa waliyo someshwa ni:

  • 1- Kuunganisha vitendo.
  • 2- Kusoma kwa vitendo.
  • 3- Kutumia zana mpya katika kufundisha.
  • 4- Njia za kisasa za ufundishaji.
  • 5- Mihadhara ya ki-itikadi.

Washiriki walisifu na kuishukuru sana Atabatu Abbasiyya tukufu kwa kuwapa semina hizi zinazo wasaidia sana katika utekelezaji wa majukumu yao ya ufundishaji, na kuwawezesha kutambua mbunu na zana za kisasa katika sekta hiyo jambo ambalo lina manufaa makubwa kwa maendeleo ya taaluma hapa Iraq.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: