Mwakilishi wa ujumbe wa bara la Asia katika kongamano la Rabiu shahada: Malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) yanajenga hisia na utukufu wa kufungamana na Imamu Hussein (a.s)…

Maoni katika picha
Katika hafla ya ufunguzi wa kongamano la kitamaduni na kimataifa Rabiu shahada awamu ya kumi na nne, lililo anza Alasiri ya leo Ijumaa (3 Shabani 1439h) sawa na (20 Aprili 2018m) kulikua na ujumbe wa washiriki wanaotoka katika bara la Asia, ulio wasilishwa na Dokta Nadhim Hussein mkufunzi wa chuo kikuu na mnadhimu wa vipindi vya luninga (tv) ya Pakistani, amesema kua: “Hakika ni utukufu mkubwa sana kwangu na ni fursa ya nadra sana kupata nafasi ya kuongea katika haram hii tukufu na katika tukio maalimu kama hili mbele ya watu watukufu kama nyie, nawashukuru sana waandalizi wa hafla hii walio nipa nafasi hii katika tukio hili na ziara hii fupi lakini sita isahau”, akabainisha kua: “Katika maisha yangu ya kazi ambayo yanafika miaka telathini, nimetembea sehemu nyingi na nimehutubia hafla nyingi, lakini ziara hii ni ya pekee katika maisha yangu yote, na kupata nafasi ya kuongea mbele ya waheshimiwa hawa walio jaa ubinadamu, sioni cha kuongea na mimi nimesimama mbele ya Imamu Hussein (a.s) na mtukufu Abbasi (a.s) katika hafla ya watu wastaarabu, acha niongee kwa hisia zangu halisi”.

Akaendelea kusema: “Katika siku chache ambazo nimekua hapa nimefanya ziara mara nyingi katika malalo mawili matatukufu, kila mara nilikua napata hisia tofauti, nilipata hisia tofauti kwa Abulfadhil Abbasi hali kadhalika naendelea kupata hisia tofauti, bado malalo hii inaendelea kutoa hisia kutokana na kufungamana kwake na Imamu Hussein (a.s), navutiwa na sifa za pekee za Abulfadhil Abbasi (a.s), alikua na upekee maalumu unaweza kuhisi hilo utakapo kua ndani ya malalo yake tukufu, hakika alikua ni kielelezo cha utiifu na kweli yeye ni mlango wa haja (baabu hawaaiji)”.

Akasisitiza kua: “Katika zama hizi za utandawazi, iwapo ulimwengu ukitafuta uislamu halisi, atachomoza Imamu Hussein (a.s) kama nuru na njia inayo faa kufatwa na watu wa imani zote, hakika heshima yake, vitendo vyake na mafundisho yake yanafika mbali zaidi ya dini, imani, utaifa, rangi na utamaduni, hakika yeye ni mwakilishi wa binadamu wote, msimamo wake ulikua dhidi ya utwaghuti na vitendo vibaya, vitendo vyake vinawakilisha mafundisho ya mitume na mawasii wote:

  • 1- Hakika yeye ni ngao ya watu wote wanao upenda uislamu katika dunia nzima.
  • 2- Hakika yeye ni msuluhishaji wa watu wote duniani.
  • 3- Hakika yeye ni mfano wa kweli katika kujitolea na kufanikisha islahi.

Watu waamke, watoke katika kughafirika kila mmoja atayaona haya.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: