Kuanza kwa vikao vya kitafiti katika kongamano la kitamaduni na kimataifa Rabiu shahada awamu ya kumi na nne…

Maoni katika picha
Asubuhi ya Juma Mosi (4 Shabani 1439h) sawa na (21 Aprili 2018m) imeanza ratiba ya vikao vya kitafiti katika kongamano la kitamaduni na kimataifa Rabiu shahada awamu ya kumi na nne, na kuhudhuriwa na viongozi wakuu wa kisheria wa Ataba mbili tukufu pamoja na makatibu wao wakuu sambamba na jopo la watafiti na wasomi wa dini na wa sekula kutoka ndani na nje ya Iraq, ndani ya ukumbi wa Imamu Hassan (a.s) katika Atabatu Abbasiyya tukufu.

Kikao kiliongozwa na Dokta Swabiih Ka’abi, kilifunguliwa kwa Qur’an tukufu, kisha ikasomwa surat Fat-ha kwa ajili ya kuwarehemu mashahidi wa Iraq, halafu zikawasilishwa tafiti zifuatazo:

  • 1- Shekh Muhammad Jawaad Lankarani kutoka katika mji wa Qum nchini Iran, utafiti wake ulikua unasema: (Harakati za Husseiniyya na mazingira halisi ya uislamu).
  • 2- Shekh Nizaar Muhammad Shauki kutoka Qatif nchini Saudia, utafiti wake ulikua unasema: (Athari ya misimamo ya kiimani katika kumjenga mpiganaji (mujahidin).. Bariri bun Khadhiir (r.a) kama mfano).
  • 3- Shekh Abbasi Ali Kaashifu-Ghitwaa kutoka Iraq, utafiti wake ulikua unasema: (Mradi wa fatwa tukufu ya kujilinda).

Tafiti hizo zimeibua mambo ambayo hayakuwahi kuzungumzwa sana siku za nyuma, na zimepata mwitikio mkubwa, ikiwa ni pamoja na michango mbalimbali kutoka kwa wahudhuriaji, na mwisho watafiti wakapewa zawadi.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: