Atabatu Abbasiyya tukufu yaweka zaidi ya ndoo za kutupia taka (1000) katika barabara zinazo elekea Karbala…

Maoni katika picha
Miongoni mwa maandalizi ya kuwapokea mazuwaru wa Imamu Hussein (a.s), Atabatu Abbasiyya tukufu kupitia Maahadi ya turathi za Mitume (a.s) imesambaza zaidi ya ndoo za kutupia taka (1000) katika barabara zinazo elekea Karbala zinazo tumiwa zaidi na mazuwaru, kwa ajili ya kusaidia kuweka mazingira ya usafi kwenye barabara hizo.

Shekh Hussein Turabi ambaye ni mkuu wa Maahadi hiyo ameuambia mtandao wa Alkafeel kua: “Hakika kazi hii ni sehemu ndogo ya kazi nyingi zilizo fanywa na Atabatu Abbasiyya tukufu katika sekta mbalimbali, na tumeanza kuweka ndoo hizi ndani ya uwanja wa haram tukufu ya Abulfadhil Abbasi (a.s) hadi katika njia zinazo tumiwa zaidi na mazuwaru, vilevile Maahadi imechukua jukumu la kufanya usafi katika baadhi ya maeneo sambamba na kusambaza ndoo za kuwekea taka.

Akaongeza kua: “Ndoo za kuwekea taka zenye ukubwa tofauti zimewekwa katika nguzo za taa zilizopo katikati ya barabara, na zimeandikwa ujumbe unao himiza kutunza usafi, tumesambaza sehemu tatu, ambazo ni:

  • 1- Barabara ya (Bagdad – Karbala).
  • 2- Barabara ya (Baabil – Karbala).
  • 3- Barabara ya (Najafu – Karbala).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: