- 1- Kuwaita mazuwaru waingie ndani ya hema la maukibu na kusoma Qur’ani ukurasa mmoja au zaidi na kuzielekeza thawabu za kisomo hicho kwa mashahidi, mwaka jana maukibu hii ilifanikiwa kusoma mamia ya khitima kwa ajili ya mashahidi wa Iraq na Hashdi Sha’abi.
- 2- Kuendesha visomo vya Qur’ani ndani ya hema au nje kwa kushirikiana na taasisi au jumuiya za Qur’an.
- 3- Kuonyesha filamu za baadhi ya matukio ya kishujaa yaliyo fanywa na wapiganaji wa Hashdi Sha’abi na namna walivyo weza kukomboa miji iliyokua imetekwa na magaidi wa Daesh.
- 4- Kugawa machapisho yenye aya za Qur’ani kwa mazuwaru.
- 5- Hema hizi hazijaishia upande wa wanaume peke yake, bali kuna hema za wanawake pia. Jambo hili linafanyika kwa mwaka wa tatu mfululizo, wanafanya usomaji wa surat Fat-ha na sura fupi fupi pamoja na nyeradi za swala chini ya walimu mahiri wenye uzowefu mkubwa, pia kuna darsa maalumu la watoto.
Kadri muda unavyo kuwa mrefu ndio tunavyo zidi kuwakumbuka na kuwatia rohoni, Mwenyezi Mungu azipe subira familia zenu na akujalieni kuwa waombezi wao siku ya kiyama na akufufueni pamoja na Imamu Hussein (a.s).