Sayyid Swafi asifu koo za waifaq kwa kuilinda Iraq na maeneo matakatifu…

Maoni katika picha
Kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya tukufu Mheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi (d.i) amesifu kazi kubwa na muhimu, iliyo fanywa na koo za wairaq katika kupambana na njama za magaidi wa Daesh walipo ivamia Iraq, akasifu pia namna koo hizo zinavyo linda na kuendeleza maadhisho ya Husseiniyya ya kudumu.

Sayyid Swafi amekutana na jopo la wazee wa ukoo wa Bani Ka’abi kutoka mkoa wa Waasit katika ukumbi wa utawala ndani ya Atabatu Abbasiyya tukufu ambapo amesema kua: “Namshukuru Mwenyezi Mungu hakika ukoo wenu -sawa na koo zingine za wairaq- mna mashahidi, mmejitolea kwa hali na mali katika kukomboa taifa hili, hii ndio desturi tukufu ya koo za wairaq zimekua na msimamo wa kupambana na magaidi wa Daesh, sawa iwe kwa kutoa watoto wao au misaada, kama ambavyo hatuwezi kusahau nafasi ya koo hizo -ukiwemo ukoo wenu- katika kuhuisha maadhimisho ya Imamu Hussein (a.s)”.

Akabainisha kua: “Katika siku za vita dhidi ya magaidi wa Daesh wana koo kupitia mawakibu Husseiniyya walifanya kazi kubwa ya kutoa huduma tukufu kwa wapiganaji, kutokana na huduma walizo wapa ndugu zao wapiganaji ziliwapa nguvu na kuwafanya wapate ushindi, tabia hii inatokana na malezi yanayo patikana katika mimbari za bwana wa Mashahidi (a.s)”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: