Kuanza kwa vikao vya mada za kitafiti katika kongamano la kimataifa kuhusu lugha ya kiarabu na fani zake

Maoni katika picha
Asubuhi ya Alkhamisi (6 Rajabu 1440h) sawa na (14 Machi 2019m) vimeanza vikao vya mada za kitafiti katika kongamano la kimataifa kuhusu lugha ya kiarabu, linalo simamiwa na Atabatu Abbasiyya tukufu kwa kushirikiana na taasisi ya Bahrul-Ulumi Aalkhairiyya chini ya kauli mbiu isemayo: (Hauza ni kitovu cha mabadiliko), na kuhudhuriwa na watafiti pamoja na wasomi wa dini na sekula kutoka ndani na nje ya Iraq, sambamba na kuhudhuria kwa kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya tukufu Mheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi.

Kikao cha mada za kitafiti cha kwanza kimefanyika ndani ya ukumbi wa Shekh Tusi kwenye jengo la taasisi (ya Bahrul Uluum Alkhairiyya) katika mkoa wa Najafu, hicho ni kikao cha kwanza katika vikao vinne vinavyo tarajiwa, vikao viwili vitakua hapa, na vingine viwili kwenye ukumbi wa Imamu Hassan (a.s) katika Atabatu Abbasiyya tukufu.

Kikao cha ufunguzi kiliongozwa na Dokta Hakim Habibu Kuraitwi na walioshiriki katika kuwasilisha mada za kitafiti ni:

  • - Dokta Rahmani Gharkani, utafiti wake unasema: (Muhammad Bahrul Ulumi katika machapisho yake).
  • - Dokta Ali Yusufu Nurudini, utafiti wake unasema: (Nafasi ya hauza ya Najafu katika kukihudumia kiarabu na wanachuoni wake mashuhuri wa zama hizi).
  • - Dokta Hiyaam Abduzaidi, utafiti wake unasema: (Athari ya hauza katika harakati za kurekebisha lugha, Shekh Karbasi kama mfano).
  • - Dokta Haidari Jabbari Idani Abu Swibii, utafiti wake unasema: (Somo la Nahau katika hauza, Shekh Muhammad Ali Mudarisi maarufu kwa (mwalimu wa kiafghani) wa mwaka 1329 – 1406h kama mfano).
  • - Dokta Jaasim Farihi Daaikh Turabi, utafiti wake unasema: (Selebasi za lugha katika hauza .. masomo na mpangilio).
  • - Ustadh Muhammad Ni’imah Samawi, utafiti wake unasema: (Najafu ni kitovu cha uboreshaji wa mashairi ya kiarabu.. Shekh Abdulhamidi Samawi kama mfano).
  • - Dokta Swabahu Anuuz, utafiti wake unasema: (Mashairi ya Sayyid Muhammad Bahrul Uluum (r.a) baina ya misingi na visa katika uhalisia wa maisha).

Kikao hiki kilikua na mwitikio mkubwa kutokana na ubora wa tafiti zake kwani zimejikita katika mambo yaliyokua hayajazungumzwa sana, na kulikua na maoni, maswali na michango mbalimbali kutoka kwa wahudhuriaji, ambapo watafiti walijibu na kufafanua pale walipo hitajika kutoa ufafanuzi zaidi.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: