Kumalizika kikao cha tatu cha mada za kitafiti katika kongamano la nne kimataifa kuhusu lugha ya kiarabu na fani zake.

Maoni katika picha
Asubuhi ya leo Ijumaa (7 Rajabu 1440h) sawa na (15 Machi 2019m) ndani ya ukumbi wa Imamu Hassan (a.s) katika Atabatu Abbasiyya tukufu, kimefanyika kikao cha tatu cha mada za kitafiti katika kongamano la nne kimataifa kuhusu lugha ya kiarabu, linalo simamiwa na Atabatu Abbasiyya kwa kushirikiana na taasisi ya Bahrul Uluum Alkhairiyya chini ya kauli mbiu isemayo: (Hauza ni kitovu cha mabadiliko).

Kikao kimeongozwa na Dokta Swabahu Abu Janaah, katika kikao hiki imesomwa mihtasari ya tafiti tisa, yafuatayo ni majina ya watafiti na zafiti zao:

  • 1- Dokta Saidi Jaasim Zubaidiy: (Msimamo wa Shekh Muhammad Jawaad Aljazaairiy katika kurahisisha nahau).
  • 2- Dokta Aamali Hussein Alwaan: (Wataalamu wa historia ya mashairi katika hauza ya Najafu karne ya kumi na mbili na kumi na tatu hijiriyya).
  • 3- Dokta Qusway Samiri Issa Alhilliy: (Selebasi ya lugha kwa wanachuoni wa hauza – Sayyid Ali bun Twauus kama mfano).
  • 4- Dokta Saamir Abdulkaadhim Jalabi: (Historia ya fani za kiarabu – Munjizu Mahmudu Bustaniy kama mfano).
  • 5- Dokta Muhammad Abdurahmaan Arifi/ kutoka Misri: (Athari ya Najafu katika kulinda lugha ya kiarabu kwa kusaidia wanachuoni na maktaba kwa ujumla).
  • 6- Shekh Imaad Kaadhwimiy / kutoka Atabatu Kadhimiyya tukufu: (Sayyid Hibatu-dini Shaharistani na mchango wake katika lugha ya kiarabu – kuonyesha usomaji kwa ufupi).
  • 7- Dokta Aatwiy Abayati / kutoka Iran: (Sifa na utenzi wa mashairi ya Najafu).
  • 8- Dokta Ali Khadwiri Haji: (Maandishi ya fani za watu wa Najafu yaliyopo katika hauza ya Najafu).
  • 9- Muhammad Munaadhil Abbasi: (Msamiati wa Nahau kwa ibun Ataaiqiy).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: