Atabatu Abbasiyya tukufu imeandaa safari ya familia za mashahidi na majeruhi ya kwenda kuzuru malalo ya bibi Zainabu (a.s).

Maoni katika picha
Atabatu Abbasiyya tukufu imeandaa safari ya familia za mashahidi na majeruhi wa Hashdi Shaábi ya kwenda kutembelea malalo ya bibi Zainabu (a.s) na Alawiyyaat katika mji mkuu wa Sirya Damaskas, kutokana na namna inavyo wajali walio itikia wito wa Marjaa Dini mkuu, waliojitolea roho zao kwa ajili ya kulinda taifa na aqida, wakafuata nyayo za kiongozi wao bwana wa mashahidi (a.s), hilo linaonekana kwa namna Ataba inavyo zijali familia za mashahidi na majeruhi wa Hashdi Shaábi, safari hii ni moja kati ya mambo mengi yanayo fanywa na Ataba kwa watu hawa.

Safari hiyo ipo chini ya usimamizi wa kikosi cha Abbasi (a.s) cha wapiganaji, tumeongea na kiongozi wao amesema kua: “Safari hii imeratibiwa na Atabatu Abbasiyya tukufu chini ya maelekezo ya kiongozi mkuu wa kisheria Mheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi (d.i), yeye ndiye alishauri kuandaa msafara wa kwenda kufanya ziara katika malalo ya bibi Zainabu (a.s) katika kumbukumbu ya kifo chake, safari hii inajumuisha familia za mashahidi walio jitoleo roho zao kwa ajili ya taifa letu tukufu, pamoja na kundi la majeruhi walio umia katika vita ya heshima na utukufu, kutokana na kuitikia kwao wito wa Marjaa uliohami taifa na maeneo matakatifu”.

Wageni wa Hauraa Zainabu (a.s) wameshindwa kuelezea hisia zao walipokua wanahuisha utiifu wao na kuhudumia mazuwaru watukufu, wameshukuru sana jambo hili tukufu walilo fanyiwa na Atabatu Abbasiyya.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: