Katika kufanyia kazi sera ya kujitegemea kwa kutumia mafundi wake: Idara ya mafundi chuma ni nguzo muhimu ya kutekeleza miradi ya Atabatu Abbasiyya tukufu.

Maoni katika picha
Idara ya mafundi chuma katika kitengo cha usimamizi wa kihandisi chini ya Atabatu Abbasiyya imesha fanya kazi nyingi za ujenzi wa majengo kwa kutumia vyuma, kazi ambazo hupita hatua mbalimbali, pamoja na kutengeneza madirisha, milango na mengineyo, nayo ni idara yenye mchango mkubwa katika kufanikisha miradi mingi ya Ataba tukufu ndani na nje ya haram takatifu.

Swafaau Adnani mmoja wa watumishi wa idara hiyo amesema kua: “Tunafanya kazi za aina tofauti ikiwemo miradi ya ujenzi pamoja na kutengeneza vitu vinavyo hitajika katika malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s)”.

Akaongeza kua: “Watumishi wa idara yetu wanafanya kazi kwa muda mrefu, kwa ajili ya kumtumikia Abulfadhil Abbasi (a.s) na mazuwaru wake”.

Fahamu kua idara ya mafundi chuma chini ya kitengo cha usimamizi wa kihandisi hufanya kazi zote zinazo husiana na chuma kwenye miradi ya Atabatu Abbasiyya tukufu kupitia mafundi wake wa sekta tofauti.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: