Muonekano wa huzuni na majonzi umetanda katika Atabatu Abbasiyya tukufu

Maoni katika picha
Huzuni na majonzi vimetanda katika Atabatu Abbasiyya tukufu, kufuatia kumbukumbu ya kifo cha Imamu Jafari Swadiq (a.s), kuta za Ataba zimewekwa mapambo meusi na zimewekwa mabango yaliyo andikwa maneno ya utiifu kwa Imamu wa sita (a.s), pamoja na maneno yanayo ashiria huzuni inayo umiza roho za wafuasi wa Ahlulbait (a.s).

Kama kawaida katika kuomboleza misiba ya watu wa nyumba ya Mtume (a.s), Atabatu Abbasiyya imeandaa ratiba maalum ya maombolezo yenye vipengele vingi, pamoja na ushiriki wake katika kuwahudumia mazuwaru, ratiba hiyo inavipengele vifuatavyo:

  • 1- Kupokea mawakibu za waombolezaji kupitia kitengo cha maadhimisho na mawakibu Husseiniyya chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu.
  • 2- Mgahawa (mudhifu) wa Abulfadhil Abbasi (a.s) umeandaa mamia ya sahani za chakula na kukigawa kwa mazuwaru kupitia madirisha ya nje.
  • 3- Kuweka vikao vya mihadhara (majlisi) ndani ya haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s).
  • 4- Kuweka majlisi maalum kwa ajili ya watumishi wa Abulfadhil Abbasi (a.s) katika ukumbi wa utawala.
  • 5- Kufanya matembezi ya kuomboleza kwa watumishi wa Abulfadhil Abbasi (a.s) kwa ajili ya kumpa pole bwana wa mashahidi Abu Abdillahi Hussein (a.s).

Fahamu kua Atabatu Abbasiyya huandaa ratiba maalum katika kila tukio linalo husu watu wa nyumba ya Mtume (a.s).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: