Idara ya miswala chini ya makumbusho ya nakala kale na vifaa Alkafeel… inatumia mbinu za zamani kwa vifaa vya kisasa katika kutunza miswala

Maoni katika picha
Idara ya miswala katika makumbusho ya Alkafeel ambayo ipo chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu inatumia mbinu za zamani kwa vifaa vya kisasa katika kurepea na kutunza miswala chini ya mafundi walio bobea katika kazi hizo.

Idara hii inatunza miswala kielimu na kwa kufuata kanuni za makumbusho katika utunzaji, kazi hiyo hupita katika hatua kadhaa, miongoni mwa hatua hizo ni:

  • 1- Kuandaa ukurasa wa maelezo (ukubwa na aina).
  • 2- Kuondoa vumbi kwenye mswala.
  • 3- Kuweka alama maalum kwenye kila mswala inaitwa (Barkod).
  • 4- Kutumia baadhi ya vitu vya asili kwa ajili ya kufukuza wadudu na nge.
  • 5- Mswala huvingirishwa kwenye bomba baada ya kuwekwa kwenye nailoni.
  • 6- Mswala ufunikwa kwa kipande cha katani.

Fahamu kua makumbusho ya vifaa na nakala kale Alkafeel ni makumbusho ya kwanza kufunguliwa katika Ataba tukufu za Iraq, ilifunguliwa mwaka (2009) katika kumbukumbu ya kuzaliwa kwa bibi Zainabu (a.s), inaidadi kubwa ya vifaa kale vyenye karne na karne.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: