Katika kuongeza uwezo wao: Kitengo cha habari na utamaduni kinaendesha semina ya kuwajengea uwezo watumishi wa kitengo cha maarifa ya kiislamu na kibinadamu

Maoni katika picha
Kwa ajili ya kuongeza uwezo wao kiutendaji na kubaini vipaji vyao, idara ya watoto na makuzi chini ya kitengo cha habari na utamaduni cha Atabatu Abbasiyya imeandaa semina kwa watumishi wa kitengo cha maarifa ya kiislamu na kibinadamu, itakayo fanyika kwa muda wa siku kumi chini ya wakufunzi walio bobea wanao weza kufundisha kutokana na uwezo wa washiriki.

Mafunzo hayo yanafanyika ndani ya ukumbi wa Qassim (a.s) katika Atabatu Abbasiyya na kusimamiwa na walimu mahiri walio peana majukumu ndani ya siku zote kumi, kila siku itakua na mada mbili au tatu, siku ya kwanza ilikua na mada zisemazo:

  • - Uandaaji wa andiko: imewasilishwa na Ustadh Swabaah Rahimah
  • - Utambulisho wa hafla: umefanywa na Ustadh mwanahabari maarufu Haidari Salami.
  • - Usanifu: imewasilishwa na ustadh Nurdini Rahmani kwa kushirikiana na Ustadh Ali Auni.

Ratiba hiyo itaendelea hadi mwisho chini ya maelekezo ya kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya tukufu Mheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi, ukiwa ni muendelezo wa kuwajengea uwezo watumishi kulingana na fani zao, ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao, semina hii ni ya kwanza kufanywa na idara ya watoto na makuzi.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: