Kumaliza hatua ya pili katika mradi wa uwekaji wa marumaru kwenye haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s) na kuingia hatua ya tatu…

Maoni katika picha
Ndani ya muda uliopangwa na kwa mujibu wa makadirio ya kiufundi, kazi ya kuweka marumaru kwenye haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s) inaendelea, baada ya kumaliza sehemu ya kwanza ya eneo la mlango wa Imamu Haadi (a.s) na mlango wa Furaat (Alqamiy), ambapo kazi hiyo imefanywa kwa ubora mkubwa, tukaingia katika sehemu ya pili, nayo imekamilika kwa wakati, ambayo ilikua ni sehemu ya kaskazini ya Atabatu Abbasiyya tukufu, katika eneo la katikati ya milango miwili, mlango wa Imamu Haadi na mlango wa Imamu Mussa Alkadhim (a.s) linalo tokea katika eneo la uwanja wa katikati ya haram mbili tukufu, na hivi karibuni tumeingia katika sehemu ya tatu ya mradi huo, ya kuweka marumaru katika eneo la katikati ya mlango wa Imamu Mussa Alkadhim (a.s) na mlango wa Imamu Hassan (a.s).

Rais wa kitengo cha miradi ya kihandisi katika Atabatu Abbasiyya Mhandisi Dhwiyaau Majidi Swaaigh ameuambia mtandao wa Alkafeel kua: “Haram tukufu ya Abulfadhil Abbasi (a.s) tumeigawa sehemu nyingi katika mradi wa kuweka marumaru, kwa namna ambayo hatuzuwii mazuwaru kuendelea na ibada zao, kila sehemu ikikamilika tunaifungua na kuhamia sehemu nyingine, tutaendelea kufanya hivyo hadi tumalize kuweka marumaru katika uwanja wote wa haram tukufu”.

Akaongeza kua: “Kazi inaendelea vizuri tunatarajia kumaliza ndani ya muda uliopangwa na kwa ubora wa hali ya juu, kazi hii inajumuisha uwekaji marumaru majengo ya chini, kwenye mitambo ya umeme, sehemu za usambazaji wa maji na sehemu ya taa na zinginezo, pamoja na kazi zingine za awali kama vile kutoa marumaru za zamani na kurekebisha sehemu zilizo haribika”.

Kuhusu wasifu wa marumaru amesema kua: “Marumaru ni za kawaida ambazo hupatikana kwa nadra (Malt Oksi), zinamazuri mengi, muhimu ni kwamba ni marumaru za kawaida zenye rangi nzuri na uwezo mkubwa wa kuvumilia mazingira, zinamuonekano mzuri na zinaupana wa (sm 4) takriban.

Kumbuka kua mradi wa kuweka marumaru kaika haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s), ni mradi unaokamilisha miradi iliyotekelezwa siku za nyuma, unafanyika baada ya kuharibiba marumaru za zamani na kuharibu mandhari ya haram kutokana na ukongwe wake, kwani zilikua zina Zaidi ya miaka mia moja tangu ziwekwe kwenye haram tukufu, pia kwa ajili ya kupendezesha sehemu hii tukufu ambayo ni miongoni mwa sehemu za peponi, kwa namna ambayo itawafurahisha mazuwaru watukufu.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: