Wito wa kushiriki kwenye kongamano la chuo kikuu Al-Ameed la kimataifa la udaktari

Maoni katika picha
Chuo kikuu Al-Ameed chini ya kamati ya malezi na elimu ya juu katika Atabatu Abbasiyya tukufu, kimetoa wito wa kushiriki kwenye kongamano la kimataifa awamu ya pili la udaktari, litakalo fanywa chini ya kauli mbiu isemayo: (Kwa tafiti za kielimu tunaweza kuhakiki mazingira salama kiafya), litafanywa chini ya usimamizi wa wizara ya elimu ya juu na tafiti za kielimu, na kwa kushirikiana na chuo kikuu cha Alkafeel na hospitali ya rufaa Alkafeel, na chuo kikuu cha UKM cha Malezia kuanzia tarehe (1 – 2 Septemba 2021m).

Kongamano litaangalia maendeleo yaliyopatikana katika sekta ya udaktari katika miaka ya hivi karibuni, sambamba na maendeleo ya kimaabara, maendeleo hayo yamewezesha kufanyika tafiti muhimu, ambazo zimesaidia kuboresha matibabu kwa kiwango kikubwa, mazingira yameruhusu chuo kikuu cha Al-Ameed kufanya kongamalo la awamu ya pili la kitabibu, ili kuendana na maendeleo hayo pamoja na kuendeleza tafiti za kielimu katika kipindi ambacho zinahitajika zaidi kwa ajili ya kupambana na janga la virusi vya Korona pamoja na magonjwa mengine.

Link ya kujisajili kwenye kongamano ni: black_small_square na mtandao maalum ni: https://conference.alameed.edu.iq/

Mada zitakazo wasilishwa kwenye kongamano hilo ni:

  • - Maendeleo ya kielimu katika sekta ya utabibu na uhandisi.
  • - Matibabu ya moyo kwa ndani.
  • - Janga la Korona na changamoto zake nchini Iraq.
  • - Maradhi ya damu.
  • - Afya ya uzazi.
  • - Uzuri wa tiba ya meno.
  • - Uuguzi wa kitanda na matibabu.
  • - Utengenezaji wa dawa.
  • - Mtazamo mpya katika huduma za afya na mafunzo ya uuguzi.

Tambua kuwa chuo kikuu cha Al-Ameed kinafanya juhudi ya kuboresha tafiti za kielimu katika sekta ya utabibu, pamoja na kusaidia kuelimisha jamii mambo ya afya, sambamba na kuweka mazingira wezeshi ya kufanya tafiti mbalimbali za kitabibu.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: