Majmaa-Ilmi imefanya mashindano ya Qur’ani katika nyumba za makazi za Abbasi.

Majmaa-Ilmi ya Qur’ani tukufu katika Atabatu Abbasiyya kupitia kituo cha miradi ya Qur’ani imeendesha mashindano ya Qur’ani ya mwezi wa Ramadhani awamu ya tatu katika nyumba za makazi za Abbasi -a.s-.

Kiongozi wa idara ya harakati katika Majmaa-Ilmi Sayyid Wahaaji Abaadi amesema “Mashindano yamehusisha vikundi (14) vya vijana wenye umri wa chini ya miaka ishirini, nayo ni miongoni mwa mashindano muhimu, yanaongozwa na majaji wenye kiwango cha juu kutoka Ataba na wanafunzi wa hauza”, akabainisha kuwa “Kazi ya kuchagua washiriki wa mashindano haya ilifanywa kwa kupitia upigaji wa kura”.

Akaongeza kuwa “Kupitia mashindano haya, kituo kinatumia vizuri mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa kusambaza utamaduni wa kusoma Qur’ani katika jamii sambamba na kufanyia kazi ndoto ya Atabatu Abbasiyya tukufu”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: