Uhuishaji wa Lailatul-Qadri ya pili na uinuaji wa misahafu mbele ya malalo ya Imamu Ali (a.s).

Makundi ya mazuwaru yamehuisha usiku wa Lailatul-Qadri wa pili, na kuomboleza kifo cha Imamu Ali Bun Abu Twalib (a.s) kwa kunyanyua misahafu mbele ya malalo yake takatifu katika mji wa Najafu.

Mji wa Najafu umeshuhudia makundi makubwa ya waombolezaji, yamekuja kufanya ziara na kusoma dua za usiku wa (21) katika mwezi wa Ramadhani (Lailatul-Qadri ya pili), na kuomboleza kifo cha Imamu Ali bun Abu Twalib (a.s).

Mazuwaru huhuisha usiku huu kwa kusoma dua maalum, kuinua misahafu, kusoma Qur’ani na kufanya (vikao) Majlisi za kuomboleza.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: