Idara ya shule za Alkafeel imeshiriki kwenye uchangiaji wa misaada kwa watu wa Iran na Lebanon

Shule za Alkafeel za kidini tawi la wanawake chini ya ofisi ya kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya, zimeshiriki kwenye uchangiaji wa misaada kwa watu wa Iran na Lebanon.

Kiongozi wa idara Bibi Bushra Alkinani amesema: “Uchangishaji wa misaada umefanywa kutokana na wito wa Marjaa-Dini mkuu, aliyehimiza kusaidia watu wa nchi hizo”.

Akaongeza kuwa “Tukio hilo limepata muitikio mkubwa, watu wengi wamekuja kutoa misaada ya kibinaadamu, jambo ambalo linaonyesha mshikamano wa kijamii, kidini na kimaadili”.

Ushiriki huo ni sehemu ya juhudi za utoaji wa misaada ya kibinaadamu zinazofanywa na Atabatu Abbasiyya kwa ajili ya kusaidia wahanga wa vita, hususan Iran na Lebanon, kwa kufanya matukio ya kukusanya misaada kwa ushiriki wa vitengo vya Ataba na taasisi zake mbalimbali.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: