Kiongozi wa idara Bibi Bushra Alkinani amesema: “Uchangishaji wa misaada umefanywa kutokana na wito wa Marjaa-Dini mkuu, aliyehimiza kusaidia watu wa nchi hizo”.
Akaongeza kuwa “Tukio hilo limepata muitikio mkubwa, watu wengi wamekuja kutoa misaada ya kibinaadamu, jambo ambalo linaonyesha mshikamano wa kijamii, kidini na kimaadili”.
Ushiriki huo ni sehemu ya juhudi za utoaji wa misaada ya kibinaadamu zinazofanywa na Atabatu Abbasiyya kwa ajili ya kusaidia wahanga wa vita, hususan Iran na Lebanon, kwa kufanya matukio ya kukusanya misaada kwa ushiriki wa vitengo vya Ataba na taasisi zake mbalimbali.



