Kikosi cha Abbasi (a.s) kimetangaza kukamilisha maandalizi ya kushiriki katika kulinda misafara ya mahujaji watakao tumia usafiri wa nchikavu (barabara).
Kikosi kimesema kuwa, kimeimarisha ulinzi magharibi ya mkoa wa Karbala kwa kuweka karibu askari elfu moja watakao hakikisha usalama wa wageni wa Mwenyezi Mungu kwa kushirikiana na vikosi vingine vya ulinzi na usalama.
Akaongeza kuwa, mkakati wa ulinzi unafanywa kwa kuweka vikosi vya askari katika vituo muhimu, kuanzia Habaria, njia panda ya Nakhibu upande wa Ramadi na Ratwaba, kuweka vituo katika jangwa la Anbaar, kufunga mitambo ya ulinzi na kuweka wanajeshi katika utayali wa kupambana na tishio lolote.
Kikosi cha Abbasi (a.s) hushiriki kila mwaka katika kulinda misafara ya mahujaji wanaotumia usafiri wa nchikavu (barabara) kwa kushirikiana na vikosi vingine vya ulinzi na usalama, jambo ambalo linasaidia wageni wa Mwenyezi Mungu kwenda na kurudi salama.



