Ameshiriki pia kiongozi mkuu wa kisheria katika Ataba Alamah Sayyid Ahmadi Swafi, baadhi ya viongozi wa Ataba na wahudumu, pamoja na kundi kubwa la walimu wa Hauza, wanafunzi, viongozi wa Dini, viongozi wa kijamii na kundi kubwa la waumini.
Waombolezaji wametaja athari kubwa iliyoachwa na mwalimu huyo wa Hauza katika mji wa Najafu, umri wake wote ameutumia katika kutumikia Dini na kusambaza elimu ya Ahlulbait (a.s).
Marjaa-Dini mkuu Muheshimiwa Ayatullah Sayyid Ali Husseini Sistani ametoa salamu za rambirambi kutokana na kifo cha Marjaa-Dini Ayatullah Shekhe Muhammad Is-haqa Alfayaadh (r.a), amepongeza mwenendo wake kielimu na mchango mkubwa aliotoa katika Hauza, na kusambaza elimu ya Ahlulbait (a.s).

































