Makamo rais wa kitengo Sayyid Ausi Twahiri amesema: “Ugawaji wa maji umehusisha mawakibu Husseiniyya zilizopo katika eneo linalozunguka haram tukufu, ambapo jumla ya katoni elfu 25 zimetolewa”.
Akaongeza kuwa “Jambo hilo ni sehemu ya huduma zinazotolewa na Atabatu Abbasiyya kwa mawakibu Husseiniyya ndani ya mwezi wa Muharam, jambo linalosaidia kurahisisha shughuli za uombolezaji kwa zuwaru wanaokuja katika mji mtukufu wa Karbala”.
Kitengo cha utumishi kinafanya kila kiwezalo katika kufanikisha ziara ya Ashura na kutoa huduma bora kwa waombolezaji.




