Kwa kushirikiana na kitengo cha maadhimisho.. Mawakibu za kuomboleza zimehuisha kumbukizi ya siku ya saba toka kuuwawa Imamu Hussein (a.s)

Mawakibu za kuomboleza kwa kushirikiana na kitengo cha maadhimisho na mawakibu Husseiniyya chini ya Atabatu Abbasiyya, zimeadhimisha kumbukizi ya siku ya saba toka kuuwawa Imamu Hussein (a.s).

Barabara zinazoelekea kwenye malalo ya Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s), zimeshuhudia mawakibu za waombolezaji zikiwa zimebeba bendera za uombolezaji na kuimba qaswida na tenzi zinazo amsha hisia za majonzi na huzuni.

Kitengo cha maadhimishi kimeandaa mkakati maalum wa kusimamia matembezi ya mawakibu, na kuteua njia maalum za kupita kila maukibu, ili kuepusha msongamano na muingiliano baina ya mawakibu na zuwaru.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: