Mradi wa upanuzi wa haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s) wa kupauwa ukumbi wake mtukufu: Umezingatia upora wa kiujenzi na huduma kwa mazuwaru.

Maoni katika picha
Kama inavyo julikana ukumbi wa haram tukufu ya Abulfadhil Abbasi (a.s) ulikua umepauliwa wote, kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri kwa mazuwaru watukufu na kuwakinga na jua pamoja na mvua, hakika huu ni miongoni mwa miradi muhimu iliyo fanywa na Atabatu Abbasiyya, na umuhimu wake ulionekana zaidi baada ya mradi wa upanuzi wa haram tukufu uliotekelezwa kwa umaridadi na ufundi mkubwa, kwa namna ambyo inaendana na ubora uliopo katika haram zingine kubwa duniani.

Paa iliyo jengwa imezingatia alama za kiislamu katika ujenzi wa haram za malalo matakatifu, tena imepambwa zaidi, kwa sababu kazi ya kuchagua aina za nakshi na mapambo ya paa na kubba tukufu imefanywa na wajenzi wa kiislamu wanaofahamu mazaru na Ataba tukufu zote, hivyo waliangalia nakshi na mapambo yaliyopo katika Ataba za zamani kisha wakachagua aina bora na nzuri na wakajenga kisasa zaidi.

Kazi hii imefanywa na mikono ya raia halisi wa Iraq, walikua na haki ya kupata nafasi hiyo na kuonyesha uwezo wao, sambamba na vifaa bora na vizuri kabisa vilivyo tumika katika utekelezaji wa mradi huu, yote hayo ni kwa ajili ya kuhakikisha tunatoa huduma bora zaidi kwa mazuwaru wa Abulfadhil Abbasi (a.s).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: