Kituo cha uzalishaji na matangazo mubashara Alkafeel ni kituo kamili cha utangazaji

Maoni katika picha
Kituo cha uzalishaji na matangazo mubashara Alkafeel ni moja ya mafanikio makubwa ya Atabatu Abbasiyya tukufu katika sekta ya utangazaji, kwani kinatangaza matukio yote ya ziara pamoja na makongamano na mikutano inayo fanywa au kusimamiwa na Ataba tukufu, kituo hicho kinavifaa vya kisasa zaidi na watumishi walio bobea katika uandishi wa habari.

Makamo kiongozi wa kituo cha uzajishaji na matangazo mubashara Alkafeel Ustadh Iswaam Mussawi amesema kua: “Lengo la kuanzishwa kituo hiki ni kufikisha ujumbe wa Atabatu Abbasiyya na miradi yake kwa walimwengu”.

Akaongeza kua: “Miongoni mwa malengo muhimu ya kuanzishwa kwa kituo hiki ni kupunguza msongamano ambao hutokea katika ziara zinazo hudhuriwa na mamilioni ya watu, kwa kupunguza idadi ya gari za matangazo ya mubashara pamoja na vyombo vya habari, sisi huandaa masafa ya kurusha matangazo mubashara bure kwa vyombo vyote vya habari vinavyo taka kurusha matukio ya ziara”.

Fahamu kua kituo cha uzalishaji na matangazo mubashara Alkafeel kutokana na kazi nzuri kinayo fanya kimekua miongoni mwa vituo bora vya utangazaji.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: