Hali inayo pitia taifa la Iraq na raia wake kwa sasa ni sababu kubwa ya kila anaye kwenda kumzuru Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s) katika usiku wa Ijumaa kuliombea taifa na watu wake.
Katika haram hizo tukufu na chini ya kubba zake takatifu, wapenzi wa Ahlulbait (a.s) wanainua mikono yao na kuomba dua chini ya kubba zake, wairaq wote wanaliombea taifa amani na usalama, wanasoma dua za aina mbalimbali huku wakitawasal kwa Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s), wanaliombea amani na utulivu taifa hili.