Kumaliza kazi ya kuweka maandishi ya Qur’ani katika sehemu ya jengo iliyowekwa Dhahabu kwenye malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s) na kuingia katika hatua inayo fuata

Maoni katika picha
Rais wa kitengo cha miradi ya kihandisi katika Atabatu Abbasiyya tukufu Mhandisi Dhiyaau Majidi Swaaigh amesema kuwa wamemaliza moja ya sehemu za mradi wa kukarabati na kuweka dhahabu katika jengo la malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s), nayo ni kazi ya kuweka maandishi ya Qur’ani ambayo yapo katikati ya pande mbili, upande wa ukuta uliofunikwa kwa vipande vya dhahabu, sehemu inayojulikana kwa jina la (Twarima) na kuelekea upande mwingine unao pakana na sehemu hiyo pamoja na kazi ya kurepea sehemu zingine zilizo baki.

Akaongeza kua: “Hatua ya kuweka maandishi ya Qur’ani ni miongoni mwa hatua muhimu katika mradi huu, mafundi wametumia nguvu zao zote kuhakikisha wanakamilisha hatua hii pamoja na hatua zingine za mradi huu, kazi ya kuweka herufi ni sawa na kazi ya kupamba, kwani inapendezesha ukuta tena kwa herufi tukufu zilizo pambwa na zenye rangi ya kupendeza, kwa kupendezesha zaidi hati zimenakshiwa kwa mapambo ya kiislamu yanayo endana na utukufu wa eneo hili”.

Kumbuka kua herufi hizo ni za aya za Qur’ani tukufu na zimewekwa sehemu tatu, ili zaairu aweze kuzisoma kwa ukamilifu, wasifu wa herufi hizo upo kama ifuatavyo:

  • - Aina ya hati ni Thuluth Jalliy iliyo shiba na kutiwa dhahabu Ayari (24) yenye viwango vitatu na ubapa wa jino la kalam (sm3.6), kazi hii imefanywa na mchoraji wa kiiraq anaeitwa Ustadh Farasi Abbasi.
  • - Ubavu wa kulia unakipimo cha (sm70 x sm351) zilizo andikwa surat Ikhlasi.
  • - Upande wa katikati mbele ya Twarima unakipimo cha (sm70 x sm700) zimeandikwa sehemu ya aya ya (177) katika surat Baqarah.
  • - Upande wa kushoto unakipimo cha (sm70 x sm 349) na zimeandikwa surat Kauthar (Innaa a’twainaakal kauthar…).
  • - Jumla ya pande zote tatu inakua ni (m14 x sm70).
  • - Vipande vya maandishi vimetiwa dhahabu halisi na kuvishwa Mina ya bluu.
  • - Maandishi yanamapambo mazuri ya kiislamu upande wa juu (sm 20) na upande wa chini kiwango hicho hicho, na vimetiwa dhahabu ya ujazo wa Ayari (24).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: