Tukio adimu sana, tangu miongo na miongo barafu hazijadondoka katika ardhi hii, Mwenyezi Mungu mtukufu ametaka barafu zidondoke katika kubba za nuru na minara mitukufu ya Karbala, Alfajiri imechanganyika na weupe wa barafu, ni hali ambayo haijawahi kushuhudiwa katika Ataba tukufu, na kuweka muonekano mwingine kwenye malalo takatifu.
Fahamu kua mji mtukufu wa Karbala upo jangwani, wakati wa majira ya joto hufika hadi nyuzijoto 45 wakati wa mchana. Na wakati wa majira ya baridi hufika hadi nyuzi joto sifuri katika baadhi za siku, mvua huathiri hali ya hewa pia kwasababu ni mji ambao umezungukwa na jangwa, lakini kwa miaka mingi haijadondoka barafu katika mji huu.