Kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya tukufu amechukua jukumu la kugharamia matibabu ya majeruhi wote wa ajali ya Sirya

Maoni katika picha
Kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya Mheshimiwa Sayyid Ahmadi Swafi amechukua jukumu la kugharamia matibabu ya majeruhi wote wa ajali iliyo tokea Sirya pembezoni mwa mji wa Damaskas, sawa majeruhi huyo anatibiwa ndani au nje ya Iraq, sambamba na kufuatilia mchakato mzima wa kusafirisha maiti, hayo yanesemwa na mjumbe wa kamati kuu ya uongozi wa Ataba Sayyid Mustwafa Dhiyaau-Dini.

Akaongeza kua: “Kuna watumishi wa Atabatu Abbasiyya waliopo Sirya wanafuatilia hatua zote za usafirishaji wa maiti na hali za majeruhi, kuna mawasiliano ya hali ya juu kwa ajili ya kuondoa vikwazo vyote na kuhakikisha majeruhi wanapata huduma za lazima kimatibabu”.

Akabainisha kua: “Hili sio jambo jipya kwa Atabatu Abbasiyya tukufu, imesha wahi kugharamia matibabu ya majeruhi wa tukio la kigaidi lililo walenga mazuwaru nchini Sirya, pamoja na kusafirisha mashahidi walio uwawa kwenye tukio hilo, japokua kulikua na mazingura magumu wakati huo”.

Katika tamko la kwanza lililotolewa na naibu katibu mkuu Ustadh Maitham Zaidi alisema kua: “Hakika uongozi mkuu wa Atabatu Abbasiyya tukufu tumewasiliana na ofisi ya waziri mkuu na muungano wa opresheni za kijeshi pamoja na wizara ya ulinzi kwa ajili ya kuandaa ndege ya kivita itakayo safirisha majeruhi na miili ya walikufa kwenye ajali hiyo, kwa kushirikiana pia na serikali ya mkoa wa Karbala, tumekamilisha maandalizi yote yanayo hitajika”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: