Muhimu: Kuwasiri miili ya watu waliokufa kwenye ajali nchini Sirya katika uwanja wa ndege wa Damaskas na maandalizi ya kuwapeleka katika nchi yao kipenzi yanaendelea

Maoni katika picha
Miili ya mazuwaru wa bibi Zainabu (a.s) wa kiiraq, waliokufa kwenye ajali nchini Sirya imewasili uwanja wa ndege wa Damaskas kwa ajili ya kuwapeleka nchini kwao, baada ya kufanyiwa ibada ya kushindikizwa (katika malalo tukufu ya bibi Zainabu –a.s-).

Ujumbe wa Atabatu Abbasiyya ulikwenda kwa anga (9 Machi 2020) katika mji mkuu wa Sirya Damaskas kushughulikia mchakato wa kusafirisha wahanga wa ajali iliyotokea pembezoni mwa mji wa Damaskas Sirya.

Mchakato huo umefanywa kwa kushirikiana na wizara ya nje ya Iraq pamoja na ubalozi wa Iraq nchini Sirya, na wizara ya ulinzi ya Iraq na uongozi wa muungano wa opresheni za kijeshi sambamba na serikali ya mkoa wa Karbala na idara ya afya ya mkoa huo.

Tambua kua maandalizi yote yamekamilika katika mji mkuu wa Sirya Damaskas chini ya ufuatiliaji wa ujumbe wa Atabatu Abbasiyya uliopo huko, ikiwa ni pamoja na vibali vya vifo na usafiri wa kuwatoa hospitali na kuwapeleka uwanja wa ndege.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: