Punguzo hilo ni sehemu ya kuonyesha kushikamana na wanafunzi wake katika mazingira haya magumu ambayo wananchi wanapitia kwa sasa, punguzo lipo kama ifuatavyo:
- 1- Ada ya masomo katika ngazi zote imepunguzwa mara ya pili kwa asilimia kumi (%10), katika mwaka wa masomo (2019/2020m).
- 2- Hivyo jumla ya punguzo katika mwaka wa masomo (2019/2020m) linakuwa asilimia ishirini (%20).
- 3- Mwanafunzi atanufaika na punguzo hilo (lililo tajwa kwenye namba moja) kwa kulipa ada kamili ya masomo kuanzia tarehe (29/04/2020m) hadi mwisho wa mda rasmi wa kazi katika siku ya Jumatano ya tarehe (20/05/2020m).
- 4- Punguzo la pili (lililo tajwa kwenye namba mbili) halihusishi wanafunzi waliopewa punguzo hapo awali kwa sababu maamum.
- 5- Wanafunzi watakao chelewa kulipa ada zao baada ya tarehe (20/05/2020m) hawatanufaika na punguzo lililotajwa kwenye namba moja.
Kumbuka kuwa chuo kikuu cha Al-Ameed kimetangaza punguzo kama hili, linalo lenga kuwasaidia wazazi wa wanafunzi, kutokana na mazingira magumu mambayo wananchi wanapitia kwa sasa.