Kwaheri.. ewe mwezi wa Ramadhani

Maoni katika picha
Utamaduni wa kila mwaka ambao Ataba mbili takatifu Husseiniyya na Abbasiyya zimekuwa zikifanya, husikika sauti za wasomaji wa dua usiku kwenye minara mitakatifu, katika siku za mwisho wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, hasa kuanzia mwezi ishirini na nane hadi mwisho wa mwezi, husomwa maneno ya kuuaga mwezi wa rehema na maghafirah, mwezi ambao ni shule na fursa ya kubadilisha tabia.

Zimesikika sauti muruwa za wasomaji, zinazo tia hisia ya huzuni kwa msikilizaji kutokana na kuuaga mwezi huu mtukufu, kama ulivyo pokewa na minara miwili mitakatifu, mnara wa bwana wa mashahidi na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s), leo unaagwa kwa maneno yanayo tia huzuni, tunamuomba Mwenyezi Mungu aurejeshe tena kwa waumini mwakani, mazingira halisi yanasema: Mwezi wa Ramadhani jua lake limekaribia kuzama, saa zake zimeisha na siku zake zimeondoka, tunauaga huenda ikawa ndio mara ya mwisho, na huenda tukakutana nao mwakani kama Mwenyezi Mungu akituandikia hivyo, alikuwa ni mgeni mwenye siku za kuhesabika, siku hizo zimeisha haraka.

Miongoni mwa beti zilizo sikika zikisomwa kwenye minara ya malalo mawili takatifu ni:

Kwaheri kwaheri ewe mwezi wa Ramadhani

Kwaheri kwaheri ewe mwezi wa kisimamo

Kwaheri kwaheri ewe mwezi wa twaa na ghufraan

Kwaheri kwaheri ewe mwezi wa wema na ihsaan
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: