Chuo kikuu cha Al-Ameed kimetandaza azma ya kufanya warsha kwa njia ya mtandao kuhusu (Utulivu wa mustakbali wa vyuo kwa kutumia zana za tafakari za aina sita)

Maoni katika picha
Chuo kikuu cha Al-Ameed kimetangaza azma yake ya kufanya warsha kwa njia ya mtandao kuhusu (Utulivu wa mustakbali wa vyuo kwa kutumia zana za tafakari za aina sita) tarehe nane mwezi Juni mbele ya muwakilishi wa waziri wa elimu ya juu na utafiti wa kielimu Mheshimiwa mkuu wa utafiti, mikakati na ufuatiliaji Dkt Ihabu Abbasi Naaji, na rais wa chuo kikuu cha Mustanswariyya Dkt. Hamiid Fadhili Tamimi.

Mkufunzi wa warsha hiyo ni (Dkt. Taqi bun Abduridhwa Abduwani) kutoka Oman, katika warsha hiyo watajadili changamoto kubwa zinazo patikana vyuoni, na mambo ya baadae au utafiti wa mustakbali, pamoja na athari za teknolojia katika soko la ajira, watajadili pia tafakari ya aina sita katika kuandaa mkakati wa chuo wa kujihami na hatari zisizo julikana.

Usajili uko wazi kwa watu wafuatao:

  • - Marais wa vyuo na mawakala wao pamoja na wasaidizi wao.
  • - Wakuu wa vitengo na mawakala wao pamoja na wasaidizi wao.
  • - Wakuu wa vitivo na idara katika vyuo vikuu vya Iraq.

Kumbuka kuwa tangu kufunguliwa kwa chuo kikuu cha Al-Ameed kimejitahidi kujenga uhusiano mzuri na vyuo vikuu vya kiarabu na kiajemi kutoka nchi mbalimbali, kama sehemu ya kuboresha mitaala ya elimu pamoja na kubadilishana uzowefu.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: