Mkuu wa kituo hicho Ustadhat Asmahani Ibrahim amesema kuwa: “Katika mazingira ya kawaida tumezowea kuwasiliana na wanafamilia pamoja na wasimamizi wa nyumba na watu wa rika zote, aidha huwa tunawapokea katika ofisi zetu na kujibu maswali yao au kutatua shida zao, lakini kutokana na mazingira ya sasa na ulazima wa kuchukua tahadhari za kiafya kwa ajili ya kujikinga na maambuizi ya virusi vya Korona, tumelazimika kutumia jukwaa la mitandao ya mawasiliano ya jamii katika kujibu maswali na kutatua shida za wadau wetu, huduma hii imepata mwitikio mkubwa”.
Akaongeza kuwa: Hivyo tumelazimika kuongeza idadi ya mitandao yetu, pamoja na wataalamu, pia tumeongeza muda wa kupokea maswali na taarifa kupitia mitandao ifuatayo:
- 1- Mtandao wa mambo ya kinafsi: https://forms.gle/YecoSuigGC9PrbGB7
- 2- Mtandao wa mambo ya familia na ndoa: https://forms.gle/aXKxPJZDqW8LhXy48
- 3- Mtandao wa vijana: https://forms.gle/joWUaHWt9dWgvkMa9
- 4- Mtandao wa watoto: https://forms.gle/GCrUmPZuGgHdkBj47