Miongoni mwa kazi za ujenzi wa kituo cha Alhayaat cha sita katika mkoa wa Muthanna: mafundi wa kitengo cha usimamizi wa kihandisi wamekamilisha ujenzi wa boma la chuma hatua ya kwanza na wameanza hatua ya pili

Maoni katika picha
Mafundi wa kitengo cha usimamizi wa kihandisi katika Atabatu Abbasiyya tukufu wamekamilisha kazi ya ujenzi wa boma la chuma sehemu ya kwanza ya ujenzi wa kituo cha Alhayaat cha sita cha kutibu watu walio ambukizwa virusi vya Korona katika mkoa wa Muthanna, na wameanza kazi ya kukata vyumba.

Bwana Swafaa Muhammad Ali Mhandisi mtendaji wa mradi huo ameuambia mtandao wa Alkafeel kuwa: “Kazi inaendelea kama ilivyo pangwa, mafundi wanatarajia kukamilisha mradi huu ndani ya muda ulio kusudiwa na kwa ubora unaotakiwa”.

Akasema kuwa: “Kazi zimefika katika hatua zifuatazo:

  • - Umekamilika ujenzi wa boma la juma katika hatua ya kwanza na tumeingia hatua ya pili.
  • - Tumeanza kazi ya kukata vyumba kwa kutumia (Sandweeg panel).
  • - Tumeanza kazi ya kumwaga zege ya hatua ya tatu na ya mwisho kwenye eneo la uwanja wa kituo.
  • - Tunaendelea na kazi ya kuweka bomba za maji taka pamoja na bomba makuu za usambazaji wa maji safi”.

Akaongeza kuwa: “Kazi zote zinaendelea kama zilivyo pangwa bila kuwepo na muingiliano wowote, aidha kazi ya kufunga nyaya za umeme pia imeanza, na ufungaji wa (jipsambord) utaanza hivi karibuni”.

Kumbuka kuwa ujenzi wa kituo hiki unaofanywa na kitengo cha usimamizi wa kihandisi chini ya Atabatu Abbasiyya unatokana na mchango wa kupambana na maambukizi ya virusi vya Korona na kuongeza uwezo wa hospitali ya Hussein (a.s) katika mkoa wa Muthanna, kituo hicho kinaukubwa wa mita za mraba (3500) kitakuwa na vyumba (114) vyenye kila kitu cha lazima katika vifaa tiba.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: